Mtekaji wa watoto Arusha, akamatwa mkoani Geita - KULUNZI FIKRA

Sunday 3 September 2017

Mtekaji wa watoto Arusha, akamatwa mkoani Geita

Polisi mkoani Geita wanamshikiliwa kijana Samson Petro (18) mkazi wa katoro wilayani Geita mkoani Geita kwa tuhuma za kuteka watoto katika mikoa ya Arusha na Geita.

Kijana huyo amekamatwa usiku wa September 2, saa mbili usiku katika nyumba ya kulala wageni ya shilungulu iliyopo mji mdogo wa katoro.

Kamanda wa polisi mkoani Geita, Mponjali Mwabulambo amethibitisha kukamatwa kwa kijana huyo na kusema polisi wanaendelea na uchunguzi na utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

1 comment:

Popular