Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Karagwe, mkoani Kagera jana ililazimika kuhamia kwa muda katika kanisa la kipentekoste la Huruma Katika Kristo kufuatia kuwepo madai ya Mchungaji wa kanisa hilo kuishi kinyumba na wake za waumini wake kwa kile anachodai kushukiwa na Roho Mtakatifu.
Mbali na kuishi na wake za waumini wake, Mchungaji huyo aliyefahamika kwa jina la Jafece Josephat anadaiwa kuwakatisha masomo baadhi ya wananfunzi katika Kijiji cha Nyakintuntu ambao wamejiunga na kanisa lake.
Kufuatia hali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Godfrey Mheluka aliamuru kukamatwa kwa mchungaji huyo alipofika kusikiliza sakata hilo kutoka pande zote mbili.
Wakati huo huo, Mkuu wa Wilaya alisema kuwa serikali itachunguza kama kanisa hilo limesajili, na ikiwa halijasajiliwa, hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa.
Mchungaji huyo na mke (Domina Damian) wa muumini wake walianza kuishi pamoja kama mke na mume kuanzia Aprili 16 mwaka huu. Sakata hilo liliibuka baada ya mume wa Domina kutaka arejeshewe mahari yake aliyokuwa ametoa kumua mwanamke huyo.
Sunday 3 September 2017
Home
Unlabelled
Mchungaji akamatwa kwa kuoa mke wa muumini wake
Mchungaji akamatwa kwa kuoa mke wa muumini wake
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment