Kwa mara nyingine tena jeshi la polisi mkoani Geita limepiga marufuku, kongamano la kuadhimisha miaka 25 ya CHADEMA lililopangwa kufanyika leo tarehe 03/09/2017 ambalo maandalizi yake yamekamilika.
Sababu zilizotolewa na mkuu wa polisi wilaya ya Geita, SSP Ally Kitumbi ni kwamba hakuna polisi wa kutosha kwa ajili ya kulinda kongamano hilo kwa kuwa polisi wapo kwenye maandalizi ya usimamizi mtihani wa darasa la saba.
Ikumbukwe kwamba polisi walizuia kongamano hili kwa mara ya kwanza tarehe 06/08/2017 kwa maelezo kuwa jeshi la Polisi lilikua katika maandalizi ya kupokea mwenge wa uhuru, na hivyo wakakosa askari wa kutosha wa kulinda kongamano hilo. Leo tena polisi wanasema hawana askari wa kutosha kulinda kongamano hilo kwa kuwa wapo kwenye maandalizi ya mtihani wa darasa la saba.
Kutokana na polisi kila mara kudai hakuna askari wa kutosha, Chadema wameomba ruhusa ya kufanya kongamano hilo bila ulinzi wa Polisi kwa kuwa maandalizi yote yamekamilika, lakini polisi wamekataa.
Sunday, 3 September 2017
Home
Unlabelled
Geita: polisi wapiga marufuku kongamano la Chadema.
Geita: polisi wapiga marufuku kongamano la Chadema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment