Kwa mara nyingine tena jeshi la polisi mkoani Geita limepiga marufuku, kongamano la kuadhimisha miaka 25 ya CHADEMA lililopangwa kufanyika leo tarehe 03/09/2017 ambalo maandalizi yake yamekamilika.
Sababu zilizotolewa na mkuu wa polisi wilaya ya Geita, SSP Ally Kitumbi ni kwamba hakuna polisi wa kutosha kwa ajili ya kulinda kongamano hilo kwa kuwa polisi wapo kwenye maandalizi ya usimamizi mtihani wa darasa la saba.
Ikumbukwe kwamba polisi walizuia kongamano hili kwa mara ya kwanza tarehe 06/08/2017 kwa maelezo kuwa jeshi la Polisi lilikua katika maandalizi ya kupokea mwenge wa uhuru, na hivyo wakakosa askari wa kutosha wa kulinda kongamano hilo. Leo tena polisi wanasema hawana askari wa kutosha kulinda kongamano hilo kwa kuwa wapo kwenye maandalizi ya mtihani wa darasa la saba.
Kutokana na polisi kila mara kudai hakuna askari wa kutosha, Chadema wameomba ruhusa ya kufanya kongamano hilo bila ulinzi wa Polisi kwa kuwa maandalizi yote yamekamilika, lakini polisi wamekataa.
Sunday 3 September 2017
Home
Unlabelled
Geita: polisi wapiga marufuku kongamano la Chadema.
Geita: polisi wapiga marufuku kongamano la Chadema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment