Msuva akimbizana na Okwi - KULUNZI FIKRA

Sunday 3 September 2017

Msuva akimbizana na Okwi

Nyota wa Taifa Stars, Saimon Msuva ameonyesha kwamba ni hatari katika kufunga baada ya kukimbizana na staa wa Simba na timu ya Taifa ya Uganda, Emanuel Okwi.

Msuva aliifungia Stars mabao yote mawili wakati ikiilaza Botswana 2-0 jana Jumamosi hivyo kufikisha idadi ya mabao matatu katika mechi mbili za mwisho alizocheza.

Kabla ya kujiunga na Stars, Msuva alitoka kuifungia timu yake ya Difaa El Jadida ya Morocco bao moja katika ushindi wa 3-1 dhidi ya CR Khemis Zemamra.

Hata hivyo Msuva anakimbizwa na Okwi ambaye amefunga mabao matano katika mechi mbili za mwisho alizocheza. Okwi aliifungia Simba mabao manne katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kuifungia Uganda bao pekee la ushindi dhidi ya Mirsi juzi Ijumaa.

No comments:

Post a Comment

Popular