Nyota wa Taifa Stars, Saimon Msuva ameonyesha kwamba ni hatari katika kufunga baada ya kukimbizana na staa wa Simba na timu ya Taifa ya Uganda, Emanuel Okwi.
Msuva aliifungia Stars mabao yote mawili wakati ikiilaza Botswana 2-0 jana Jumamosi hivyo kufikisha idadi ya mabao matatu katika mechi mbili za mwisho alizocheza.
Kabla ya kujiunga na Stars, Msuva alitoka kuifungia timu yake ya Difaa El Jadida ya Morocco bao moja katika ushindi wa 3-1 dhidi ya CR Khemis Zemamra.
Hata hivyo Msuva anakimbizwa na Okwi ambaye amefunga mabao matano katika mechi mbili za mwisho alizocheza. Okwi aliifungia Simba mabao manne katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kuifungia Uganda bao pekee la ushindi dhidi ya Mirsi juzi Ijumaa.
Sunday, 3 September 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
No comments:
Post a Comment