Nyota wa Taifa Stars, Saimon Msuva ameonyesha kwamba ni hatari katika kufunga baada ya kukimbizana na staa wa Simba na timu ya Taifa ya Uganda, Emanuel Okwi.
Msuva aliifungia Stars mabao yote mawili wakati ikiilaza Botswana 2-0 jana Jumamosi hivyo kufikisha idadi ya mabao matatu katika mechi mbili za mwisho alizocheza.
Kabla ya kujiunga na Stars, Msuva alitoka kuifungia timu yake ya Difaa El Jadida ya Morocco bao moja katika ushindi wa 3-1 dhidi ya CR Khemis Zemamra.
Hata hivyo Msuva anakimbizwa na Okwi ambaye amefunga mabao matano katika mechi mbili za mwisho alizocheza. Okwi aliifungia Simba mabao manne katika ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kuifungia Uganda bao pekee la ushindi dhidi ya Mirsi juzi Ijumaa.
Sunday 3 September 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment