Mahujjaj 35 wafariki dunia Macca - KULUNZI FIKRA

Sunday 3 September 2017

Mahujjaj 35 wafariki dunia Macca

Wizara ya Afya na Idadi ya Watu ya Misri, imesema, Mahujjaj 35 wa nchi hiyo wamefariki dunia wakati wa siku ya kwanza ya Hijja iliyomalizika nchini Saudi Arabia kutokana na uchovu na umri mkubwa.

Afisa mmoja wa Wizara hiyo, Ahmed el Ansary, amesema umri wa Mahujjaji waliofariki ni kati ya miaka 60 hadi 85.
Katika Ibada ya Hijja ya mwaka huu zaidi ya Mahujjaj milioni mbili walihudhuria wakiwemo milioni 1.8 kutoka nje ya nchi .

No comments:

Post a Comment

Popular