WAKATI benchi la ufundi Simba likifurahia kuona viungo wake wakifunga mabao, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limelitangaza ratiba mpya ambapo pambano la watani, Simba na Yanga sasa litapigwa Oktoba 28 Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam badala ya Oktoba 14.
Katika mabadiliko hayo mechi zilizopagwa zichezwe kesho Jumatano sasa zitachezwa wikiendi huku pambano la marudiano la watani litasubiri ya hatma ya timu hizo katika michuano ya kimataifa japo inaonyesha zitacheza Machi 14 mwakani.
Msimu huu Simba imepiga hesabu kali ambazo pengine zitawaacha midomo wazi Yanga.
Simba ilifanya tathmini na kugundua ikibaki tu kuwategemea mastraika, haitaweza kutwaa taji la Ligi Kuu Bara, hivyo ikaweka nguvu pia katika eneo la kiungo.
Washindi hao wa Kombe la FA wameanza kuipoteza Yanga kwa kuwekeza katika eneo hilo ambapo viungo wake wanajua kuzifumania nyavu tofauti na Yanga inayowategemea zaidi mastraika; Amissi Tambwe, Ibrahim Ajibu, Obrey Chirwa na Donald Ngoma.
Simba licha ya kuwa na mastraika watatu; Juma Liuzio, Nicholas Gyan na Laudit Mavugo, imeweka nguvu kwa mawinga na viungo ambao wakiingia kwenye boksi tu umelia.
Viungo hao wanaofanya vizuri ni Mohammed Ibrahim, Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla na Emmanuel Okwi anayemudu pia kucheza straika.
Tuesday, 5 September 2017
Home
Unlabelled
Simba, Yanga uso kwa uso oktoba 28
Simba, Yanga uso kwa uso oktoba 28
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment