Kambi rasmi ya upinzani Bungeni imesusia kuapishwa kwa wabunge saba wa viti maalum kutoka chama cha Cuf.
Wabunge hao wameapishwa leo septemba 5 na spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania, Job Ndugai.
Wakati wabunge hao wakitoka ndani ya ukumbi wa Bunge,baadhi ya wabunge walibaki kushuhudia wabunge wa Cuf wakiapishwa wabunge waliobaki kutoka mambo rasmi ya upinzani ni Magdalena Sakaya (Kaliua), Maftah Nachuma (Mtwara mjini) na Maulid Mtulia ( kinondoni)
Awali, wafuasi wa Cuf walifika asubuhi katika viwanja vya Bunge kushuhudia kuapishwa kwa wabunge hao walioteuliwa hivi karibuni na Tume ya Taifa uchaguzi ( NEC).
Wafuasi hao waliambatana na Mbunge wa Bunge la Afrika mashariki, Habibu Mnyaa walifika wakiwa kwenye magari matatu aina ya Toyota coaster na mengine madogo yaliyokuwa yamebandikwa licha za mwenyekiti wa wa Cuf, Ibrahimu Lipumba anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini.
Wabunge wa viti maalum walioapishwa leo ni Alfredina Kiangi, Kiza Mayeye, Huru Bafadhili ,Rukia Kassima, Shamsia Mtamba, Sonia Magogo na Zainab Amir.
Hindu Mwenda ambaye angeapishwa leo alifariki dunia ijumaa ya septemba mosi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuzikwa jumapili ya septemba 3.
Tuesday, 5 September 2017
Home
Unlabelled
Kambi ya Upinzani Bunge wasusia kuapishwa kwa wabunge wapya wa cuf
Kambi ya Upinzani Bunge wasusia kuapishwa kwa wabunge wapya wa cuf
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment