Kambi rasmi ya upinzani Bungeni imesusia kuapishwa kwa wabunge saba wa viti maalum kutoka chama cha Cuf.
Wabunge hao wameapishwa leo septemba 5 na spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania, Job Ndugai.
Wakati wabunge hao wakitoka ndani ya ukumbi wa Bunge,baadhi ya wabunge walibaki kushuhudia wabunge wa Cuf wakiapishwa wabunge waliobaki kutoka mambo rasmi ya upinzani ni Magdalena Sakaya (Kaliua), Maftah Nachuma (Mtwara mjini) na Maulid Mtulia ( kinondoni)
Awali, wafuasi wa Cuf walifika asubuhi katika viwanja vya Bunge kushuhudia kuapishwa kwa wabunge hao walioteuliwa hivi karibuni na Tume ya Taifa uchaguzi ( NEC).
Wafuasi hao waliambatana na Mbunge wa Bunge la Afrika mashariki, Habibu Mnyaa walifika wakiwa kwenye magari matatu aina ya Toyota coaster na mengine madogo yaliyokuwa yamebandikwa licha za mwenyekiti wa wa Cuf, Ibrahimu Lipumba anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini.
Wabunge wa viti maalum walioapishwa leo ni Alfredina Kiangi, Kiza Mayeye, Huru Bafadhili ,Rukia Kassima, Shamsia Mtamba, Sonia Magogo na Zainab Amir.
Hindu Mwenda ambaye angeapishwa leo alifariki dunia ijumaa ya septemba mosi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuzikwa jumapili ya septemba 3.
Tuesday 5 September 2017
Home
Unlabelled
Kambi ya Upinzani Bunge wasusia kuapishwa kwa wabunge wapya wa cuf
Kambi ya Upinzani Bunge wasusia kuapishwa kwa wabunge wapya wa cuf
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment