Shaka afunguka mazito juu ya ya uchaguzi wa UVCCM Taifa. - KULUNZI FIKRA

Saturday 2 September 2017

Shaka afunguka mazito juu ya ya uchaguzi wa UVCCM Taifa.

 
 YALIYOSEMWA NA KAIMU KATIBU MKUU UVCCM SHAKA HAMDU SHAKA WAKATI AKIZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI JUMAMOSI SEPT. 2, 2017 UVCCM MAKAO MAKUU

"Dhana ya Demokrasia ni jambo muhimu linalohitaji kuheshimiwa na kuenziwa ndani ya Chama na Jumuiya zake." Amesema Shaka

"Zoezi la uchaguzi kwenye ngazi kuanzia ngazi ya tawi mpaka kata limefanikiwa vyema" Amesema Shaka

"Jumla ya Matawi 23,529 sawa na Asilimia 99.4% kati ya Matawi 23,670 sawa na asilimia 0.59 yamekamilisha uchaguzi." Amesema  Shaka

"Ngazi za Kata 3,913 sawa na Asilimia 96.59% kati ya Kata 4,051 sawa na asilimia 3.4% zimekamilisha uchaguzi." Amesema Shaka

"Kwa upande wa majimbo ya Zanzibar majimbo 54 sawa na Asilimia 100%, wamekamilisha uchaguzi." Amesema Shaka

"Jumla ya Vijana 7,606 wamejitokeza kuchuka fomu za kugombea nafasi mbali mbali katka Jumuiya yetu".Amesema  Shaka

"Kwa upande wa ngazi ya Taifa Vijana 350 wamejitokeza kuomba nafasi za uongozi ndani ya UVCCM" Amesema Shaka

"Watu 113 wamejitokeza kuomba nafasi ya Mwenyekiti, Watu 24 wameomba nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Watu 103 nafasi 5 Halmashauri kuu."Amesema  Shaka

"Watu 81 wameomba nafasi 5 Wajumbe Baraza Kuu; Watu 14 wameomba nafasi 1 uwakilishi UWT; Watu 15 wameomba nafasi 1 uwakilishi Wazazi" Amesema  Shaka

"Ni mwiko kwa mgombea kuanza kampeni mapema au kujipitisha na kuelezea nafasi anayogombea." Amesema Shaka
"Sifa za wagombea zitaandaliwa kwenye kitabu na kugawia kwa wajumbe siku ya mkutano" Amesema Shaka

"Tunaviomba vyombo vinavyohusika katika ngazi zote hasa TAKUKURU kufuatilia kwa karibu nyendo za wagombea na wapiga kura." Amesema Shaka

"UVCCM imestushwa na hali inayoonekana kutaka kuibua migogoro na kujenga mazingira ya mvurugano au kuporomoka kwa mshikamano wetu." Amesema  Shaka

"CCM si genge la wahuni. Ni Chama makini cha Siasa kinacho heshimu utu wa mtu, taratibu, miongozo katika kushughulikia mambo yake" Amesema Shaka

"Tumeanza kuwafatilia kwa karibu mno na kuanza kuwatambua wote ambao wanashiriki vitendo vya aibu vya kuchafuana ndani UVCCM na CCM" Amesema  Shaka

"Mwenye madai, tuhuma au shutuma anatakiwa atumie vikao halali vya kikanuni na kikatiba kwa kufuata utaratibu si kinyume na hivyo" Amesema Shaka

"Mwana UVCCM muadilifu, msemakweli, mpenda Umoja na Mshikamano, huheshimu kanuni, katiba na maelekezo yanayotolewa na viongozi wetu" Amesema Shaka

""Tusingependa kuona Watu wanabeba agenda binafsi au kufikiria kumchafua mtu ndio kupata cheo ndani ya UVCCM, hawatavumiliwa tena" Amesema Shaka

"Tunapaswa kuonyesha kutii, kufuata maelekezo yanayotolewa mara kwa mara na Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa Dkt. Magufuli."Amesema Shaka

"Kila Mwanachama anapaswa kujitambua, kujiheshimu, kufuata misingi ya katiba na kulinda kwa nguvu zake zote heshima ya CCM." Amesema Shaka

No comments:

Post a Comment

Popular