Mmoja kati ya wabunge 8 wateule kutoka Chama cha Wananchi CUF Bi. Hindu Hamis Mwenda amefariki dunia.
Taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa habari na mawasiliano wa chama hicho Abdul Kambaya imesema kuwa Bi Hindu amefariki katika hospitali ya taifa Muhimbili jana jioni alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa siku kadhaa.
Taarifa hiyo haijaeleza kwa undani chanzo cha kifo hicho, lakini amesema taratibu nyingine zinazofuata zitaelezwa baadaye.
Wabunge hao wapya wa viti maalum pamoja na marehemu, waliteuliwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada waliokuwa wakishika nafasi hizo kuvuliwa ubunge kutokana na kuvuliwa uanachama na hivyo kupoteza sifa ya kuwa wabunge.
Mwanzoni mwa wiki hii Spika wa Bunge Job Ndugai alitamka kuwa wabunge hao wapya wataapishwa katika kikao cha kwanza cha mkutano ujao wa bunge utakaoanza Septemba 5 mwaka huu.
Saturday, 2 September 2017
Home
Unlabelled
Mbunge mpya wa Cuf, Bi Hindu Mwenda afariki dunia
Mbunge mpya wa Cuf, Bi Hindu Mwenda afariki dunia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment