Mmoja kati ya wabunge 8 wateule kutoka Chama cha Wananchi CUF Bi. Hindu Hamis Mwenda amefariki dunia.
Taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa habari na mawasiliano wa chama hicho Abdul Kambaya imesema kuwa Bi Hindu amefariki katika hospitali ya taifa Muhimbili jana jioni alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa siku kadhaa.
Taarifa hiyo haijaeleza kwa undani chanzo cha kifo hicho, lakini amesema taratibu nyingine zinazofuata zitaelezwa baadaye.
Wabunge hao wapya wa viti maalum pamoja na marehemu, waliteuliwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada waliokuwa wakishika nafasi hizo kuvuliwa ubunge kutokana na kuvuliwa uanachama na hivyo kupoteza sifa ya kuwa wabunge.
Mwanzoni mwa wiki hii Spika wa Bunge Job Ndugai alitamka kuwa wabunge hao wapya wataapishwa katika kikao cha kwanza cha mkutano ujao wa bunge utakaoanza Septemba 5 mwaka huu.
Saturday, 2 September 2017
Home
Unlabelled
Mbunge mpya wa Cuf, Bi Hindu Mwenda afariki dunia
Mbunge mpya wa Cuf, Bi Hindu Mwenda afariki dunia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
No comments:
Post a Comment