Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema watu waliopanga na kutekeleza shambulio la risasi dhidi ya mwanasiasa machachari wa upinzani, Tundu Lissu watajulikana muda si mrefu.
Ameliambia Mwananchi kwa njia ya simu akiwa Nairobi, Kenya, alipokwenda kusimamia matibabu ya Lissu kuwa shambulio hilo lilipangwa kwa muda mrefu na kwamba waliofanya hivyo hawawezi kujificha tena.
“Tukio hili lilipangwa na kuratibiwa kwa muda mrefu. Kuna magari mengi yamekuwa yakimfuatilia Lissu kwa muda mrefu na hili jambo halikupangwa na mtu mmoja, limepangwa na watu wengi na baada ya muda kila kitu kitajulikana,” alisema.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama Cha Mawakili Tanganyika (TLS) alishambuliwia kwa risasi zaidi ya 30 nyumbani kwake Area D mjini Dodoma muda mfupi baada ya kutoka kwenye ukumbi wa Bunge.
Watu wasiofahamika walilifuatilia gari lake tangu alipotoka bungeni saa saba mchana na alipofika nyumbani kwake alisita kushuka baada ya kuona gari hilo likiendelea kumfuata na ndipo aliposhambuliwa.
Tuesday, 12 September 2017
Home
Unlabelled
Mbowe: Waliomshambulia Lissu watajulikana muda siyo mrefu
Mbowe: Waliomshambulia Lissu watajulikana muda siyo mrefu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment