Mbunge wa Tunduma akamatwa na polisi mahakamani - KULUNZI FIKRA

Tuesday 29 August 2017

Mbunge wa Tunduma akamatwa na polisi mahakamani

Mbunge wa Tunduma,Frank Mwakajoka amekamatwa na jeshi la polisi akiwa katika viwanja vya mahakama ya wilayani ya mbozi mjini vwawa.
Mwakajoka amekamatwa leo Agosti 29 baada ya kufika mahakamani hapo kwa kufuatilia kesi inayomkabili Mbunge wa mwenzake wa Mbozi,Pascal Haonga.
Katibu wa chadema wilaya ya Mbozi,James Mbasha amesema Mbunge huyo amekamatwa lakini hajui kosa linalomkabili.
Mbasha amesema amepata taarifa leo asubuhi kwamba mbunge huyo anatafutwa na polisi.
Katika kesi mahakamani hapo, Haonga na wenzake wawili Wilfred Mwalusanya na Mashaka Mwamposhi wanakabiliwa na mashtaka mawili, kufanya vurugu na kuwazui askari kufanya kazi yao kinyume na sheria.
Mwendesha mashtaka wa polisi,Samweli Saro anadai Jana,Agosti 28 saa saba mchana, washtakiwa walimzuia askari kutimiza majukumu yake ya kumkamata Masha Mwamposhi aliyedaiwa kwamba si mjumbe halali katika uchaguzi wa mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa Mlawo.
Washtakiwa wanadaiwa pia kumfanyia vurugu msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Mbozi,Lauteri kamao.
Washtakiwa walikana mashtaka mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo,Asha Waziri ambaye alisema dhamana iko wazi kwa kila mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho kutoka kwa mtendaji wa maeneo yao watakao weka bondi ya sh 2 milioni kila mmoja .
Washtakiwa walitimiza masharti na kuachiwa guru kwa dhamana,Kesi itatajwa September 25 na washtakiwa watasomewa Maelezo ya awali.

No comments:

Post a Comment

Popular