Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Enduimet (WMA) imekabidhi Sh99 milioni kwa vijiji 11 wilayani Longido kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya wananchi.
Fedha hizo zimetolewa na kampuni ya uwindaji ya Shangri-la iliyopo wilayani Longido mkoani Arusha.
Imeelezwa kuwa fedha hizo zinatokana na mapato yaliyokusanywa kwa ajili ya shughuli za uwindaji katika kampuni hiyo.
Vijiji hivyo 11 vinavyounda jumuiya hiyo kwa kutoa maeneo ya shughuli za uwindaji kila kimoja kimepewa Sh9 milioni.
Mkuu wa Wilaya ya Longido, Daniel Chongolo amewaagiza watendaji wa vijiji husika kuhakikisha wanaainisha mapato na matumizi ya fedha hizo katika kila kijiji ili zijulikane zilivyotumika.
Chongolo amesema kumekuwepo ubadhirifu wa fedha za wananchi unaofanywa na watendaji wanaojali masilahi binafsi ikiwemo kujilipa posho.
Sunday, 27 August 2017
Home
Unlabelled
Longido: Kampuni ya uwindaji yatoa million 99 kwenye vijiji 11
Longido: Kampuni ya uwindaji yatoa million 99 kwenye vijiji 11
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment