Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhil Nkurlu amesema kamati ya ulinzi na usalama imekamilisha utaratibu wa kuwasaka wanafunzi wenye mimba ili kuchukua hatua.
Aliitoa kauli hiyo juzi akiwa Kata ya Ntobo katika Halmashauri ya Msalala wakati wa makabidhiano ya mradi wa maendeleo ya jamii wa ADP Busangi uliokuwa ukitekelezwa na shirika la World Vision Tanzania kwa kuishirikisha wananchi.
Alisema pamoja na mafanikio ya mradi huo, Nkurlu ambye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, alisema kwa sasa tayari utaratibu wote kupitia kamati zote za ulinzi na usalama za mji, Msalala na Ushetu zimekaa na kukubaliana kuwasaka shule hadi shule wasichana watakao kuwa na mimba.
“Baada ya kukubaliana kitakaochofuata ni kuwakamata na wale watakaobainika hatua kali zitachukuliwa, Serikali haiwezi kutumia fedha nyingi kwa ajili ya watoto kwenda shule lakini yanafanyika mambo kinyume,” alisema.
Kaimu mkurugenzi wa shirika hilo, Johnson Robinson alisema utekelezaji wa mradi huo umeiinua sekta ya elimu.
Sunday 27 August 2017
Home
Unlabelled
DC Kahama:Tunawasaka wanafunzi wote wenye mimba na tunawachukulia hatua kali
DC Kahama:Tunawasaka wanafunzi wote wenye mimba na tunawachukulia hatua kali
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
No comments:
Post a Comment