Baraza la uongozi wa chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) limewataka mawakili nchi nzima kuto kwenda mahakamani siku ya jumanne na jumatano kama njia ya kupinga kampuni ya IMMMA Advocates kuvamiwa.
Akizungumza leo jumapili, Rais wa TLS, Mhe Tundu Lissu amesema uamuzi huo umefikiwa Jana na kikao cha baraza la uongozi la chama hicho.
Amesema mawakili wote wanaotetea wananchi kwenye mahakama na kwenye mabaraza wasifanye kazi siku hizo.
Amesema baraza hilo linafahamu kwamba Wateja wao wataathirika siku hizo lakini usalama wa mawakili ni muhimu zaidi.
Lissu amesema baraza la uongozi linavitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwahakikishia ulinzi mawakili was IMMMA Advocates dhidi ya vitisho vinavyoweza kuatarisha usalama wao.
Amesema baraza hilo linafanya jitihada za kukutana na mkuu wa jeshi la polisi na Idara ya usalama ili kujadiliana kuhusu shambulio hilo.
Lissu amewataka wananchi kuhakikisha wanalinda usalama, Uhuru na heshima ya wanasheria na mawakili ili waweze kutekeleza wajibu wao wa kuwatetea wananchi.
Sunday 27 August 2017
Home
Unlabelled
Lissu ataka mawakili wasiende mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano
Lissu ataka mawakili wasiende mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
No comments:
Post a Comment