Baraza la uongozi wa chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) limewataka mawakili nchi nzima kuto kwenda mahakamani siku ya jumanne na jumatano kama njia ya kupinga kampuni ya IMMMA Advocates kuvamiwa.
Akizungumza leo jumapili, Rais wa TLS, Mhe Tundu Lissu amesema uamuzi huo umefikiwa Jana na kikao cha baraza la uongozi la chama hicho.
Amesema mawakili wote wanaotetea wananchi kwenye mahakama na kwenye mabaraza wasifanye kazi siku hizo.
Amesema baraza hilo linafahamu kwamba Wateja wao wataathirika siku hizo lakini usalama wa mawakili ni muhimu zaidi.
Lissu amesema baraza la uongozi linavitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwahakikishia ulinzi mawakili was IMMMA Advocates dhidi ya vitisho vinavyoweza kuatarisha usalama wao.
Amesema baraza hilo linafanya jitihada za kukutana na mkuu wa jeshi la polisi na Idara ya usalama ili kujadiliana kuhusu shambulio hilo.
Lissu amewataka wananchi kuhakikisha wanalinda usalama, Uhuru na heshima ya wanasheria na mawakili ili waweze kutekeleza wajibu wao wa kuwatetea wananchi.
Sunday, 27 August 2017
Home
Unlabelled
Lissu ataka mawakili wasiende mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano
Lissu ataka mawakili wasiende mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment