Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai, amewataka mawaziri wapya walioapishwa hapo jana Oktoba 9 kujiandaa kuchapa kazi kwa nguvu zote, kwani wakati uliopo sio wa kuzembea.
Kauli hiyo ya Ndugai ameitoa jana alipokuwa akiwapongeza Mawaziri hao, ambao awali wengine walikuwa wabunge wa kawaida na sasa kuveshwa kofia za uwaziri, na kwamba wakienda bungeni ni kuchapa kazi kwani walishapata uzoefu miaka miwili iliyopita tangu awamu ya tano iingie madarakani.
"Mheshimiwa Rais ni matumaini ya watanzania kwamba timu hii ambayo inaimarisha Baraza la Mawaziri, na kama tulivyoambiwa hapa wanaanza kazi leo leo kwa kikao cha Baraza la Mawaziri, tunawatakia kila la heri, tunawakiribisheni bungeni, niwaambie neno moja tu mbele yako Mheshimiwa Rais wajiandae, hawa walioapishwa na hawa wengine waliokuwepo, hii miaka miwili ya mwanzo tulikuwa tunachukulia wanajifunza, sasa hivi tukienda Dodoma ni kazi tu", amesema Spika Ndugai.
Hapo Jana Rais Magufuli ameapisha Baraza la Mawaziri baada ya kulifanyia mabadiliko Oktoba 7, na kuwataka waanze kazi mara moja, huku wakikabidhiana nyaraka za ofisi tayari kwa utekelezaji.
Tuesday, 10 October 2017
Home
Unlabelled
Spika Ndugai: Wajiandae kwenda na kasi ya Rais Magufuli
Spika Ndugai: Wajiandae kwenda na kasi ya Rais Magufuli
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment