Rais John Pombe Magufuli amefunguka na kuzungumzia juu ya ndege za Tanzania sita zilizonunuliwa na serikali ikiwepo Bombardier Q 400-Dash ambayo inashikiliwa nchini Canada na kusema ndege hizo zitawasili nchini mwakani 2018.
Rais Magufuli amesema hayo alipokuwa kwenye Mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) ambao uliofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, Rais Magufuli amesisitiza kuwa Tanzania inakosa watalii wengi kutokana na kukosa ndege.
"Tumenunua ndege sita ndege mbili zimeshawasili Tanzania, lakini ndege zingine ikiwepo Bombardier zitawasilia mwakani 2018 mwanzoni tunafanya haya kwa ajili ya kutengeneza Tanzania mpya, nchi ambazo zina ndege zake idadi ya watalii wanaoingia kwenye nchi hiyo ni kubwa zaidi, nchi yetu ni ya pili kwa kuwa na vivutio vingi duniani lakini idadi ya watalii wanaoingia ni ndogo kutokana na kukosa ndege zetu" alisema Rais Magufuli
Serikali ilikiri ndege mpya aina ya Bombardier Q-400 Dash 8 iliyonunuliwa na serikali ambayo ilipaswa kuingia nchini toka mwezi Julai lakini ikashindikana kufika kutokana na kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd iliyozuia ndege aina ya bombardier Q400-Dash 8 iliyonunuliwa na Tanzania nchini Canada.
Tuesday, 3 October 2017
Home
Unlabelled
Rais Magufuli atoa ufafanuzi juu ya Bombardier inayoshikiliwa
Rais Magufuli atoa ufafanuzi juu ya Bombardier inayoshikiliwa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment