Viongozi wanne wa Cuf wamefariki kwenye ajari wakitokea Dodoma - KULUNZI FIKRA

Wednesday 6 September 2017

Viongozi wanne wa Cuf wamefariki kwenye ajari wakitokea Dodoma

 Viongozi wanne wa Chama cha Wananchi CUF wamefariki dunia baada ya msafara wao kupata ajali maeneo ya Ubenazomozi Mkoa wa Pwani.

Ajali hiyo imetokea jana usiku wakati Viongozi hao wakitokea Dodoma kwenye sherehe za kuapishwa kwa Wabunge wapya wa Chama hicho.

Habari zilizotufikia asubuhi hii ya leo Jumatano September 6, 2017 ni kwamba Viongozi wanne wa Chama cha Wananchi CUF wamefariki dunia baada ya msafara wao kupata ajali maeneo ya Ubenazomozi Mkoa wa Pwani. Ajali iliyohusisha gari aina ya Noah na Lori katika eneo la Ubena barabara ya Morogoro Mkoani Pwani.

Ajali hiyo imetokea jana usiku wakati Viongozi hao wakitokea Dodoma kwenye sherehe za kuapishwa kwa Wabunge wapya wa Chama hicho baada ya gari lao kugongana na Lori.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Habari wa CUF Abdul Kambaya Viongozi waliofariki ni kutoka Wilaya ya Muheza, Tanga ambapo miongoni mwao ni Mgombea Udiwani wa Muheza Mjini, aliyefahmika kwa jina moja Uredi.

Aidha, idadi ya majeruhi haijajulikana ila inasadikika kuwa  hawazidi 10 na baadhi yao wapo Hospital ya Tumbi huku akisema chanzo cha ajali hiyo ni gari la wafuasi hao kugongana na lori.

No comments:

Post a Comment

Popular