Mwenyekiti wa chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida mashariki, Tundu Lissu amepigwa risasi leo Alhamis, nyumbani kwake na kwamba hali yake ni mbaya
Lissu ambaye ni mwanasheria mkuu wa chadema na Rais wa chama cha wanasheria Tanganyika ( TLS) kwa sasa amepelekwa kwenye chumba cha upasuaji katika hospitali ya Rufaa ya Dodoma.
Katibu wa Bunge, Dkt Thomas Kashilillah, wabunge na viongozi wengine wa ulinzi wa Bunge wamegika katika hospitali hiyo kujua kinachoendelea.
Baadhi ya ndugu na wagonjwa wamefurika katika chumba cha upasuaji cha hospitali ya mkoa wa Dodoma wakitafakari huku wengine wakilia.
Mganga mkuu wa mkoa wa Dodoma, Charles Kihologwe amewataka watu hao kukaa mbali na chumba cha upasuaji lakini wengine wamekataa wakisema hawamwamini mtu yeyote.
Asubuhi, Lissu alihudhulia kikao cha Bunge na aliomba mwongozo kwa Naibu spika akihoji kuhusu taarifa za kamati zilizoundwa na spika wa Bunge, Job Ndugai, kutathimini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya Tanzanite na Almasi kuwasilishwa kwa Waziri mkuu badala ya kujadiliwa na Bunge kwanza.
Thursday, 7 September 2017
Home
Unlabelled
Tundu Lissu apigwa risasi Dodoma na hali yake ni mbaya
Tundu Lissu apigwa risasi Dodoma na hali yake ni mbaya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment