Ripoti za madini: Tundu Lissu amuwakia spika Ndugai - KULUNZI FIKRA

Thursday 7 September 2017

Ripoti za madini: Tundu Lissu amuwakia spika Ndugai

 
 Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni Mh.Tundu Lissu amemuwakia Spika kuvunja kanuni za bunge katika uwasilishaji wa ripoti za kamati mbili za madini.

Tundu Lissu anasema Spika amepokea ripoti mbiombio kuipeleka kwa Rais kabla ya kujadiliwa na wabunge ili ipelekwe kwa serikali ikiwa na maazimio ya bunge

 Lissu amesema kanuni za bunge ziko wazi na ripoti zote za kamati na tume za kibunge huwasilishwa kwanza bungeni kujadiliwa na wabunge na kupokea maoni yao. Ameshangaa kuona ripoti inakimbizwa kwa rais wakati uchunguzi ulitokana na azimio la bunge na sio rais

 Kwa hiyo wabunge wangepata nafasi ya kuchambua ripoti ile na kutoa maoni yao kwa serikali ndipo Spika angetakiwa kuwasilisha kwa rais
    

No comments:

Post a Comment

Popular