Kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa (TFF), Jamal Malinzi na wenzake wawili imeahirishwa baada ya hakimu anayesikiliza shauri hilo kuwa na dharura.
Wakili wa Serikali, Faraj Ngokah ameieleza Mahakama ya Hakimu Kisutu leo Alhamis, kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na Hakimu anayesikiliza shauri hilo, Wilbard Mashauri ana udhuru.
"Washtakiwa wapo Mahakamani, lakini Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri ana dharura, hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili kutajwa" alidai wakili Ngokah.
Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa aliahirisha kesi hiyo September 21 mwaka huu itakapotajwa.
Mbali na Malinzi, washitakiwa wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga.
Washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha.
Thursday, 7 September 2017
Home
Unlabelled
Kesi ya Malinzi yasogezwa mbele tena
Kesi ya Malinzi yasogezwa mbele tena
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment