Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P 2643, DAR ES SALAAM
Simu: +255 22 2135747/8; 2137125; 2135222
Faksi: +255 22 2111281
B/Pepe: chragg@chragg.go.tz
Tovuti: www.chragg.go.tz
Septemba 8, 2017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tamko la THBUB kuhusu Mhe. Tundu Lissu (Mb) kupigwa risasi
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imesitushwa na kusikitishwa na kitendo cha Mhe. Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika kupigwa risasi, tukio lililotokea Septemba 7, 2017 mjini Dodoma.
Tume inalaani vikali kitendo hicho kwani ni kitendo cha uvunjifu mkubwa wa sheria na haki za binadamu.
Tukio hili ambalo limekuja siku chache tu baada ya tukio la ofisi za wanasheria wa IMMMA zilizoko jijini Dar es Salaam kulipuliwa kwa bomu siyo la kawaida, na limeleta hofu siyo kwa familia ya Mhe. Tundu Lissu pekee, bali kwa wananchi wengi nchini.
Isitoshe, matukio haya hayaleti picha nzuri kwa nchi inayoheshimu demokrasia, haki za binadamu na utawala bora.
Hivyo, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora:
1. Inalitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linakamilisha haraka upelelezi wa tukio hilo na kuwapeleka wahusika katika vyombo vya sheria.
Tume inaamini kuwa iwapo wahusika wa tukio hili watachukuliwa hatua kali itasaidia kukomesha vitendo vya aina hii vinavyofanywa na makundi ya watu wanaojichukulia sheria mkononi ambayo yanaonekana kujitokeza hivi karibuni.
2. Aidha, inapenda kukumbusha kuheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora na kuepuka ukiukwaji wa Katiba na sheria za nchi.
3. Mwisho, inamtakia Mhe. Tundu Lissu kila la kheri katika matibabu yake ili apone haraka.
Imetolewa na:
(SIGNED)
Mhe. Bahame Tom Nyanduga
Mwenyekiti
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Septemba 8, 2017
Friday, 8 September 2017
Home
Unlabelled
Tume ya haki za binadamu na Utawala bora yalaani kitendo cha Tundu Lissu kupigwa risasi
Tume ya haki za binadamu na Utawala bora yalaani kitendo cha Tundu Lissu kupigwa risasi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
No comments:
Post a Comment