Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema amesikitishwa na kushambuliwa Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu tukio alilosema halijawahi kutokea nchini.
Amesema anampa pole Lissu na kumwombea kwa Mungu amjalie afya na kupona haraka ili aendelee na kazi yake ya kuwatetea wananchi.
Pia, kutetea haki na utawala wa sheria na kupambana na dhuluma, uonevu na hasa dhidi ya wanyonge.
"Tukio hili ni la kusikitisha, ni ushahidi mwingine unaoonyesha nchi yetu inaelekea kubaya. Hali hii inapaswa kudhibitiwa,” amesema.
Maalim Seif amesema leo Ijumaa kuwa, “Bila hatua madhubuti kuchukuliwa za kuiepusha nchi na chuki na kulipizana visasi miongoni mwa wananchi, mambo hayo husababisha machafuko."
Katibu Mkuu huyo wa CUF aliyewahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema pamoja na kauli za Serikali kuwa inawasaka wahalifu, anaisihi itumie uwezo wake wote kuwatia mikononi watu waliohusika katika kipindi kifupi kijacho ili wananchi waimarishe imani yao kwa Serikali.
Amesema kuna haja ya uongozi wa Tanzania kuandaa na kuitisha mkutano wa mashauriano ya kitaifa ili kushauriana namna ya kuzuia mgawanyiko nchini.
"Nampa pole Lissu na familia yake, uongozi wa Chadema na wananchi wa Singida Mashariki, pia wananchi wote walioguswa na shambulio hili la kikatili," amesema Maalim Seif.
Lissu aliyeshambuliwa kwa kupigwa risasi tano, mbili kwenye miguu, mbili tumboni na moja mkononi anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan mjini Nairobi, Kenya alikopelekwa jana Alhamisi.
Friday, 8 September 2017
Home
Unlabelled
Maalim Seif: Hili la Lissu halijawahi kutokea
Maalim Seif: Hili la Lissu halijawahi kutokea
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment