Salum Mwalimu: Hakuna raia anayeweza kumdhuru Lissu nje ya uwanja wa siasa - KULUNZI FIKRA

Thursday 7 September 2017

Salum Mwalimu: Hakuna raia anayeweza kumdhuru Lissu nje ya uwanja wa siasa

 
 Akihojiwa na idhaa ya sauti ya america (VOA) Naibu katibu mkuu wa Chadema mh Salum Mwalimu ametanabaisha maadui wakubwa wa Lissu na alishatolea taarifa polisi lakini hakuna kilichofanyika.

Mwalimu kasema hata ikiwa ni usiku akikutana na majambazi au vibaka wakijua ni Lissu hawawezi mfanya chochote atapita salama na wanaweza kumpa ulinzi hadi atakakofika.

Mara kadhaa viongozi wa serikali na chama cha mapinduzi wamekuwa wakimtolea kauli za vitisho na wengine kifikia kuomba ridhaa ya kumdhuru au kumuua lakini kwakiwa ni wana ccm hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na vyombo vya usalama.

Amekumbushia habari ya hivi karibuni kwa gari dogo lililokuwa likimfatilia dar lakini hakuna hatua zozote zilizochujuliwa wala hata kutolea ufafanuzi na polisi.

Amesema iko wazi amekuwa mwiba kwa serikali na chama tawala na amekamatwa mara nyingi na kufunguliwa kesi nyingi mwisho wa siku huachiwa.

Na kesi nyingi ni dhidi ya serikali ya ccm na liko wazi adui mkubwa wa Lissu ni serikali na akiwa akitetea maslai ya walio wengi, na hawapendi kusikia ukweli.

Kahoji kama waziri alitolewa bastola mchana na anajulikana mpaka leo hajakamatwa tusitarajie chochote katika hili la Lissu.

Imma advocate walionwa wakasema hawakuwa wao ila kuna waliovalia sare za polisi ila wako kimya mpka leo.

Wao kama chama hawana jeshi ila taarifa za watu wasio julikana ishakuwa kama habari za uchochezi hutokea upande usio wa serikali na ccm tu ndo kauli hizo hutolewa

No comments:

Post a Comment

Popular