Simba imerejea mazoezini leo kuiwinda Mwadui watakayokutana nayo Jumapili kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, huku kocha msaidizi wa kikosi hicho, Jackson Mayanja akilia na safu ya ushambuliaji.
Timu hiyo ilitoka sare na Azam katika mchezo wa Jumamosi na jana kocha Joseph Omog aliwapa mapumziko wachezaji wake na leo wamerejea tena mazoezini kujiandaa na mchezo ujao.
Mazoezi hayo pia yamehudhuriwa na mshambuliaji Emmanuel Okwi na beki Juuko Murshid ambao hawakucheza mchezo dhidi ya Azam kutokana na kuchelewa kujiunga na timu wakitokea kwenye majukumu ya timu yao ya Taifa ya Uganda Cranes.
Kukosekana kwa Okwi kulionekana kuwachanganya mashabiki wa Simba ambao wameweka imani kubwa kwa mchezjai huyo na kuamini kuwa uwepo wa mchezaji huyo kikosini unakuwa mwiba kwa timu pinzani.
Mayanja alisema bado wataendelea kukazania suala la umaliziaji kwa washambuliaji wake ili kuhakikisha timu hiyo inafunga mabao kila mechi.
"Kila mara tumeona maendeleo katika safu ya ushambuliaji ingawa bado kuna tatizo hivyo tutaendelea kulifanyia kazi tatizo la ufungaji ili kuhakikisha mechi zijazo timu inafunga na kupata ushindi.
"Licha ya kwamba kazi ya kufunga ni ya washambuliaji lakini hatutajikita kwao pekee bali kwa wachezaji wote kuhakikisha wanafunga wakipata nafasi. Tunataka tukomeshe tatizo la kukosa mabao na kuhakikisha kila nafasi inayopatikana inatumika ipasavyo ili timu ipate ushindi," alisema Mayanja.
Monday, 11 September 2017
Home
Unlabelled
Mayanja zaidi kuililia safu ya ushambuliaji
Mayanja zaidi kuililia safu ya ushambuliaji
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment