Hashim Rungwe anashikiliwa na polisi. - KULUNZI FIKRA

Tuesday 5 September 2017

Hashim Rungwe anashikiliwa na polisi.

Aliyekuwa Mgombea Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Hashimu Rungwe anashikiliwa na polisi kwa siku nne sasa.

Rungwe ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Chauma anashikiliwa katika kituo kikuu cha cha polisi kanda maalumya Dar es salaam.

Mwanasiasa huyo anashikiliwa kwa kosa la kughushi nyaraka.

Kamanda wa polisi kwa kanda maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa  amedhibitisha hayo leo septemba 5 kuwa Rungwe anashikiliwa kwa siku nne .

Hata hivyo, Kamanda Mambosasa hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo alisema ana taarifa za kutosha.

No comments:

Post a Comment

Popular