Wanachama 1,216 wa klabu ya Simba, leo Jumapili wamepitisha uamuzi wa klabu yao kuanza kuendeshwa kwa mfumo wa hisa.
Katika uamuzi huo ni mwanachama mmoja pekee ndiye alionyesha hisia zake kwa kupinga mfumo huo.
Wanachama bado wataendelea kubaki kuwa wamiliki wa klabu hiyo kwa asilimia 50 huku wawekezaji nao wakilimiliki kwa asilimia 50 pia.
Mabadiliko yaliyopitishwa na wanachama wa Simba yako hivi, wanachama watamiliki klabu yao kwa asilimia 50 huku 50 zikimilikiwa na wawekezaji.
Wawekezaji au mmoja, wawili au watatu watatakiwa kutoa Shilingi bilioni 20 katika uwekezaji huo, sawa na wanachama.
Kwa wanachama, kwa kuwa wanaonekana si wenye uwezo wa kutosha kifedha, wao watatakiwa kuchangia Shilingi bilioni nne tu ambazo ni asilimia 10 huku 40 ambayo ni bilioni 16 zitawekwa kando kwa kuangalia uwezo wao.
Suala la nani atakuwa mwekezaji itaundwa kamati baada ya watu kujitokeza, nayo itaandaa mkutano kuwaita wanachama kuwaeleza waliojitokeza katika uwekezaji huo ni kina nani.
Wawekezaji wanaweza kuwa wawili, watatu au vinginevyo na mgawanyo wa hisa kwa maana ya thamani na asilimia ndiyo utakaohusika.
Sunday, 20 August 2017
Home
Unlabelled
Wanachama wa simba sc wapitisha mfumo wa
Wanachama wa simba sc wapitisha mfumo wa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment