Kamati ya Bunge ya Bajeti imesema itaendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa njia ya kielektroniki kwa kuwa mfumo huo umeonyesha mafanikio.
Akizungumza leo Agosti 28 baada ya kamati kutembelea Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), mwenyekiti wake, Hawa Ghasia ameipongeza kampuni ya Maxcom kwa ubunifu.
Amesema kabla ya utaratibu wa malipo kwa njia ya kielektroniki fedha za Serikali zilikuwa zikipotea, hivyo kukwamisha maendeleo ya nchi.
“Napongeza kwa ubunifu huu, njia hii ya ukusanyaji mapato inatakiwa kuigwa na taasisi zote na wafanyabiashara,” amesema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Maxcom Africa Plc,Jameson Kasati amesema wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa kadi za malipo ya mabasi yaendayo haraka.
Amesema kwa sasa wananchi waendelee kutumia tiketi za kawaida na kadi zitakuwa tayari hivi karibuni.
“Kadi za mabasi yetu zitakuwa tayari hivi karibuni, endeleeni kutumia tiketi,” amesema.
Monday, 28 August 2017
Home
Unlabelled
Wabunge kusimamia mfumo wa kielektroniki
Wabunge kusimamia mfumo wa kielektroniki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment