uongozi wa juu wa chadema unaongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam - KULUNZI FIKRA

Friday, 18 August 2017

uongozi wa juu wa chadema unaongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam

Naomba nizungumzie athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje" - Tundu Lissu

=> Wanasheria wanaoishauri Serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa - Lissu

=> Ndege iliyotarajiwa kuwasili mwezi uliopita mpaka sasa haijafika na Serikali ipo kimya

=> Ndege hiyo iliyotarajiwa kufika mwezi uliopita imekamatwa na inashikiliwa Canada na wadeni wetu

=> Baada ya Waziri wa mambo ya nje kwenda Canada, Kampuni hiyo imekubali kuiachia ndege hiyo kwa malipo ya awali

=> Dkt. Mahiga alifanya ziara Canada,akiwa na Balozi wa TZ Canada,Jack Zoka,walifanya mazungumzo na Stirling Civil Engineering Ltd

=> Mazungumzo yao yalihusu deni la USD 38,711,479 inayodaiwa TZ kutokana na hukumu 2 za Mahakama ya Usuluhishi zilizotolewa 2009/10

=> Mazungumzo hayo pia yalihusu amri ya kukamatwa mali zote za TZ zilizopo mikononi mwa kampuni ya kutengeneza ndege ya Bombadier

=> Kwanini hilo deni halikulipwa mpaka miaka saba baadae ambapo deni hilo limeongezeka

=> Msisitizo wa Waziri wa mambo ya nje kutaka jambo hili liwe kimyakimya ni kwa ajili ya kumlinda nani?

=> Waziri Mbarawa alimjibu Zitto kuhusu ndege hiyo lakini hakusema ni taratibu zipi ambazo zimechelewesha ndege hiyo kuletwa

=> Nasema si kwasababu napenda kuyasema, ni kwasababu nalazimika kuyasema.

=> Baada ya Waziri wa mambo ya nje kwenda Canada, Kampuni hiyo imekubali kuachia ndege hiyo kwa malipo ya awali.

=> Tunaiomba Serikali iweke hadharani kesi zote ambazo tumeshitakiwa kwenye kesi za usuluhishi nje ya nchi.

=> Yote ambayo tumeyasema tuna ushahidi wa nyaraka, tuna nyaraka za kuthibitisha kila tulichokisema.

=> Kuna watanzania Wazalendo waliomo ndani ya Serikali hiihii ambao wametupa hizi nyaraka

=> Mimi ni mwanasheria natakiwa nisitaje chanzo lakini mjue tuna nyaraka za kuthibitisha kila tulichokisema

=> Suala la kukamatwa kwa Bombadier ya Magufuli linaibua maswali mengi yanayohitaji majibu ya Rais na Serikali yake

=> Rais Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi, kampuni ya Stirling Civil Ltd iliwahi kupewa kandarasi ya mradi wa barabara Wazo Hill - Bagamoyo

=> Kabla ya kukamilisha kandarasi hiyo, ikavunjwa mikataba bila kuzingatia sheria kampuni hiyo ilinyang'anywa kandarasi

=> Stirling Civil Engineering Ltd, ikafungua mashtaka katika Mahakama ya kimataifa ya Usuluhishi

=> Mnamo 10 Desemba 2009 na baadae 10 Juni 2010, Mahakama ya usuluhishi ilitoa tuzo ya USD 25M na riba 8% hadi malipo yatakapofanyika

=> Kampuni ya Acacia imetoa notisi ya kuishitaki serikali ili kudai fidia ya USD bilioni 2 kwa kukamata mchanga wa dhahabu -

=> Siyo Acacia peke yake, hata kampuni ya Anglo-Gold Ashanti pia ime-file notisi ya kutushtaki

=> Mtu yeyote msomi anayesema tusiogope kushtakiwa, huyo mtu haipendi Tanzania, kwa maamuzi kama haya, ukishtakiwa, umefilisika

=> Yote ambayo tumeyasema, tuna ushahidi wa nyaraka, bahati nzuri kuna watanzia wazalendo serikalini ambao wametupa hizo nyaraka

=> Lissu adai kuwa ndege ya ATCL iliyopaswa kuwasili nchini mwezi Julai 2017, imekamatwa nchini Canada na watu wanaoidai serikali ya Tanzania

No comments:

Post a Comment

Popular