Wakili wa kujitegemea na mmiliki mwenza wa Smile Stars Attorneys, Leonard Tungaraza Manyama amepinga wito uliotolewa na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kutaka wanachama wote wa TLS kususia kwenda mahakamani kwa siku mbili.
Akiongea na waandishi wa habari Leonard Tungaraza Manyama amepinga wito huo na kuwataka Wanachama wote wa TLS kuendelea na shughuli zao kama kawaida na amewataka watendaji wa TLS kutoigeuza taasisi hiyo kama chama cha siasa au taasisi inayoendesha shughuli zake kwa mtindo wa kiharakati na badala yake kibaki kwenye majukumu yake ya kutoa huduma kama taasisi ya kitaaluma.
Aidha Manyama amesema yeye kama mwanasheria na mwanachama wa TLS, amesikitishwa na tukio la shambulizi kwenye ofisi za IMMMA Advocates na kuitaka TLS kutoa muda kwa vyombo vya dola kuendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Mbali na hilo Manyama amedai mawakili na wanasheria ni watumishi wa idara ya mahakama na kwamba tukio lolote la kutofanya kazi katika siku mbili hizo kutaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wa kipato cha chini ambao wamekuwa wakihangaika kutafuta haki zao kwa muda mrefu, huku mpango wa kuhakikisha kesi za muda mrefu zinapunguzwa mahakamani nao ukikwama.
Leonard Tungaraza Manyama ameibuka siku moja baada ya Rais wa TLS Tundu Lissu kuwataka mawakili kutohudhuria kwa siku mbili shughuli za mahakama Jumatatu na Jumanne kama ishara ya kulaani tukio la shambulizi lililofanywa kwenye ofisi za kampuni ya mawakili ya IMMMA Advocates usiku wa kuamkia Agosti 26 mwaka huu.
Monday 28 August 2017
Home
Unlabelled
Tundu Lissu apingwa vikali, aambiwa asigeuze TLS kwa chama cha siasa
Tundu Lissu apingwa vikali, aambiwa asigeuze TLS kwa chama cha siasa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment