Sumaye afunguka kuhusu mashamba yake - KULUNZI FIKRA

Tuesday 22 August 2017

Sumaye afunguka kuhusu mashamba yake

Waziri mkuu mstaafu wa serikali ya awamu ya tatu,Frederick Sumaye amesema kunyang'anywa mashamba yake si sababu ya yeye kufikiria kurudi CCM.
"Kunyang'anywa mashamba yangu najua ni uamuzi wa juu haunidhoofishi nifikirie kurudi CCM"
Sumaye amesema mashamba yaliyofutwa na serikali yalikuwa yanalipiwa kodi na yalikuwa yanamilikiwa kisheria.
"Wanataka nirudi CCM, Mimi sitaki kurudi CCM, kwanini wanalazimisha? Nilisema sababu ya kuondoka huko,waseme wazi sababu za kutafuta ni za kisiasa tu"' amesema Sumaye leo katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Popular