Nimeiona Barua kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuvitaka Vyama vya siasa vitoe maoni kuhusu utungwaji wa Sheria Mpya ya Vyama vya Siasa. Nilijua kwamba jambo hili lingefuata. Serikali inachukua hatua hii wakati huu ili kubariki "UJINGA" wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa siku za usoni.
Lengo kubwa kuliko yote ni kuweka kipengele kitakachoeleza kuwa "Msajili wa Vyama vya Siasa anaweza kuingilia mambo ya ndani ya vyama vya siasa na kwamba uamuzi wake utakuwa wa mwisho."
Yaani, kumlinda mtu mmoja, LIPUMBA, ili aimalize CUF, kunafanya hadi sheria zibadilishwe haraka ili AIBU zinazofanywa na Msajili zilindwe.
Tumewahi kuwaeleza huko nyuma mara kadhaa, kwamba Mahakama Kuu imewahi kutamka bayana katika maamuzi mbalimbali, kuwa "Msajili wa Vyama vya Siasa hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya vikao vya vyama vya siasa kwa njia yoyote ile."
CUF ilipoanza kupigwa vita na LIPUMBA akiwa mtumiwaji mkuu, wapo watu walitucheka. Tuliwaambia shambulio dhidi ya CUF ni shambulio dhidi ya demokrasia.
Tusubiri wapitishe hiyo sheria yao, uone vyama vitakavyoporwa uhuru wa ndani. Na huko ndiko CCM inapenda twende, maana yanyewe haiwezi kuguswa na Msajili ambaye obvious anateuliwa na Mwenyekiti wa CCM.
#NOTE; Hata ikitungwa sheria hii hivi sasa, mashauri ya CUF yaliyoko mahakamani yatatumia viwango vya mamlaka ya msajili yaliyotajwa kwenye Sheria Namba 5 ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 (sheria ya sasa).
Tuesday, 29 August 2017
Home
Unlabelled
Mtatiro: Msajiri anataka kubadili sheria ili awe na mamlaka ndani ya vyama vya siasa
Mtatiro: Msajiri anataka kubadili sheria ili awe na mamlaka ndani ya vyama vya siasa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
No comments:
Post a Comment