Katibu Mkuu wa Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga, Charles Boniface Mkwasa amekiri kuwa klabu yao inadaiwa kodi na serikali huku akiwataka mashabiki na wanachama wa jangwani kuwa watulivu katika kipindi hiki.
Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa.
Mkwasa amebainisha hayo leo baada ya taarifa kuwepo taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu jengo lao kupigwa mnada siku ya Jumamosi
“Ni kweli tuna deni kubwa tunadaiwa na ardhi lakini tayari tulifanya nao mazungumzo na kukubaliana namna ya kulilipa kupitia mapato yetu ya milangoni. Tatizo ni kwamba hapa katikati ligi ilisimama, lakini hivi karibuni inaanza na tutaendelea kulipa, Tutatoa taarifa rasmi baadaye”, alisema Mkwasa.
Mkwasa amesema kiasi wanachodaiwa ni kikubwa lakini hakizidi shilingi milioni 500, huku akiweka wazi kuwa pesa wanayotakiwa kulipa kwa mwaka ni shilingi milioni 59.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia kwa kampuni ya udalali ya Msolopa Investmenst Limited leo imetangaza kulipiga mnada jengo hilo endapo Yanga hawatalipa kabla ya Agosti 19, mwaka huu.
Thursday, 17 August 2017
Home
Unlabelled
Mkwasa afunguka kuhusu Jengo lao
Mkwasa afunguka kuhusu Jengo lao
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
No comments:
Post a Comment