Mbunge Bunda Mjini Ester Bulaya amepata dhamana kwa mashariti ya wadhamini watu na Tsh mil 20, amepewa rufaa ya kwenda Muhimbili kwa ajili matibabu zaidi.
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Mara Joyce Sokombi (CHADEMA) amezungumzia hali ya Mbunge Mh. Ester Amos Bulaya, na kusema kwamba hali yake bado haijatengemaa kwani amepewa rufaa kwenda hospitali ya mkoa, hivyo amewataka watanzania kumuombea.
Akizungumza na mwandishi wa East Africa Radio, Mh. Sokombi amesema presha ya Ester Bulaya ambaye ni Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini bado ipo chini, kiasi kwamba wameshindwa kumsafirisha kwenda hospitali kubwa, hivyo wanasubiri madaktari wamsaidie kurudisha hali ya presha yake, ndipo wamtoe hospitali.
Pia Mh. Sokombi amesema kwa sasa Bulaya ameshapatiwa dhamana akiwa hapo hospitalini, lakini hawajajua hatma ya kesi kwani mpaka sasa hawajapewa maelezo ya sababu iliyofanywa ashikiliwe na polisi.
Monday, 21 August 2017
Home
Unlabelled
Mbunge wa Bunda mjini, Esther Bulaya apata dhamana na pia apewa rufaa kwenda hospitali ya mkoa wa Mara,haki haijatengemaa
Mbunge wa Bunda mjini, Esther Bulaya apata dhamana na pia apewa rufaa kwenda hospitali ya mkoa wa Mara,haki haijatengemaa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment