Mbunge wa Arusha,Godbless Lema akamatwa kwa madai ya kuzidisha muda wa mkutano - KULUNZI FIKRA

Wednesday 23 August 2017

Mbunge wa Arusha,Godbless Lema akamatwa kwa madai ya kuzidisha muda wa mkutano

Mbunge wa Arusha mjini Mhe.Godbles Lema amekamatwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa madai ya kuzidisha muda katika mkutano wake kwa dakika saba (07).

Polisi wanadai Lema amemaliza mkutano saa 12:07 jioni badala ya saa 12:00 kamili kama ilivyo utaratibu.

Polisi "wamemblock" Lema katika "keepleft" cha mnara wa saa kwa kusimamisha gari mbili (moja mbele na nyingine nyuma), kisha kuingia katika gari ya Lema na kumuelekeza kituo kikuu cha polisi (central).

Hali hii imesababisha foleni kubwa kwenye barabara zinazoingia katikati ya mji.

No comments:

Post a Comment

Popular