Mara,Tarime: Mtuhumiwa ajinyonga kwa kutumia shati lake mahabusu - KULUNZI FIKRA

Wednesday 23 August 2017

Mara,Tarime: Mtuhumiwa ajinyonga kwa kutumia shati lake mahabusu

 
Mkazi wa Kijiji cha Kerende Kata ya Kemambo wilaya ya Tarime mkoani Mara, Mussa Martine 17 amekutwa amekufa katika kituo cha polisi cha Nyangoto wilayani humo kwa kile kinachodaiwa kujinyonga.

Kwa mujibu wa mmoja wa majirani. Juma Nkome, marehemu alikuwa akiishi na bibi yake, alikutwa amejinyonga juzi kwa kutumia shati lake usiku wa kuamkia Agosti 22.

Inadaiwa kwamba alishikiliwa na polisi Agosti 21 kwa tuhuma za kujihusisha na tukio la ubakaji lililotokea miezi miwili iliyopita.

Kamanda wa Polisi Tarime/Rorya Henry Mwaibambe hakupatika kuzungumzia tukio hilo baada ya simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa.

No comments:

Post a Comment

Popular