Maafisa wa Libya wamethibitisha kuwa, wamemtia nguvuni kiongozi wa kundi la Daesh ambaye alikuwa akilifanyia kazi shirika la ujasusi la Israel, Mossad.
Maafisa wa Libya wamesema kuwa, Myahudi huyo aliyejulikana kwa jina la "Abu Hafs" alikuwa imamu wa jamaa wa msikiti mmoja katika mji wa Benghazi na kwamba baada ya uchunguzi imebainika kuwa, ni raia wa Israel na jina lake halisi ni Benjamin Efraim. Maafisa wa serikali ya Libya wameongeza kuwa, Efraim alikuwa akikifanyia kazi kikosi cha Mossad cha Wayahudi waliojifanya Waarabu na kufanya ujasusi katika nchi za Kiarabu na Kiislamu kwa maslahi ya Israel. Wameongeza kuwa, jasusi huyo alikuwa mwanachama wa kundi la kigaidi la Daesh na aliweza kuhamia katika mji wa Benghazi kupitia kwa kundi hilo na kuwa imamu wa Swala za jamaa.
"Abu Hafs" yaani Benjamin Efraim, alikuwa kiongozi wa wapiganaji 200 wa kundi la kigaidi la Daesh ambao wanatambuliwa kuwa makatili zaidi kuliko magaidi wengine wa kundi hilo.
Maafisa wa serikali ya Libya wanasema, lengo la kundi hilo lilikuwa kupata ushawishi na badaye kuhamishia vita na mapigano katika nchi jirani ya Misri.
Sunday, 27 August 2017
Home
Unlabelled
Libya yamkamata jasusi wa Massod Aliyekuwa kiongozi wa kidini
Libya yamkamata jasusi wa Massod Aliyekuwa kiongozi wa kidini
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment