BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limethibitisha kuwa lina mpango wa kuhamisha makao yake makuu kutoka Kurasini jijini Dar es salaam kwenda Dodoma. Hayo yameelezwa na Makamu wa Rais wa TEC ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya, wakati wa Misa Takatifu ya kilele cha jubilei ya miaka 100 ya upadri Tanzania, iliyofanyika katika kituo cha hija cha Mbwanga, Dodoma.
Akitoa salamu za TEC katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya waamini, Askofu Kinyaiya amesema kuwa baraza lina mpango wa kuhamisha makao yake makuu yaende Dodoma na mchakato huo utaanza baada ya kufanya mazungumzo na serikali ya kupata ardhi itakayotumiwa na shughuli za TEC.
“Tuna mpango wa kuhamisha makao yetu makuu yaje Dodoma. Bado tunaongea na serikali ili tupate kipande cha ardhi, ambapo leo pia tumebariki jiwe la msingi la kikanisa kitakachojengwa mahali hapo” ameeleza Askofu Kinyaiya.
Kwa upande wake mwakilishi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sherehe hizo, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene, ametoa agizo kwa serikali ya Mkoa wa Dodoma ihakikishe inafanya mazungumzo na TEC ili ndani ya siku 10 kiwanja kiwe kimepatikana kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Makao Makuu ya TEC.
"Maamuzi ya kubariki jiwe la msingi la kikanisa cha TEC kama ishara ya kuhamia Dodoma ni ujumbe mzito kwa serikali ya awamu ya tano na serikali ya Dodoma.Ninaagiza ndani ya siku kumi zoezi la upatikanaji wa kiwanja sehemu wanapohitaji liwe limekamilika.Sisi tutawapa kila aina ya msaada kwa haraka.nasi sana Dodoma title ushirikiano" ameeleza awali akitoa salami za mkoa wa Dodoma, mkuu wa mkoa huo Jordan Rugimbana amesema kuwa TEC imebariki wazi la Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli la kuhamishia makao makuu ya nchi mkoani Dodoma.
Aidha Rugimbana amesema kuwa serikali ya mkoa huo itatoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa makao makuu hayo mapya ya TCE.
Sunday, 20 August 2017
Home
Unlabelled
Baraza la maaskofu katoliki kuhamia Dodoma
Baraza la maaskofu katoliki kuhamia Dodoma
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
No comments:
Post a Comment