Kesi ya jinai inayowabili vigogo wa Chadema akiwamo mwenyekiti Freeman Mbowe kesho inaanza kuunguruma katika hatua ya usikilizwaji wa awali, upande wa mashtaka utatoa picha kamili
Mbali na mbowe wengine ni Katibu Mkuu, Dkt Vicent Mashinji na manaibu katibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).
Wengine ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake la chama hicho (Bawacha), Esther Matiko na Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee pamoja na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.
Washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 12 ya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali na ya uchochezi wa uasi, wakidaiwa kutenda makosa hayo Februari 16, 2018 wakati wa maandamano yaliyosabasha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.
Wakati kesho vigogo hao wa Chadema watakapopandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuna mambo makubwa mawili yanayotarajiwa kuyojiri katika kesi hiyo.
Jambo la kwanza linalotarajiwa kutokea kabla ya mambo yote ni kuunganishwa nao kwa mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya.
Bulaya ambaye ni mmoja wa washtakiwa katika kesi hiyo, alikuwa bado hajakamatwa na kuhojiwa kabla ya kupandishwa kizimbani kama ilivyokuwa kwa wenzake, lakini April 13, aliitwa Kituo Kikuu cha Polisi na kuhojiwa kabla ya kuachiwa kwa dhamana.
Baadaye Katibu Mkuu wa Chadema, Mashinji alilieleza Mwananchi kuwa mbunge huyo ataunganishwa nao katika kesi yao kesho.
Hivyo, ikiwa kesho atafikishwa mahakamani, basi ataunganishwa na wenzake katika kesi hiyo na katika kufanya hivyo upande wa mashtaka ulazimika kubadili hati ya mashtaka ili kuwasilisha hati ya mashtaka yenye majina ya washtakiwa wote akiwemo Bulaya.
Jambo la pili litakalojiri kesho ni usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo. Katika hatua hii upande wa mashtaka utawasomea washtakiwa mashtaka yanayaowakabili na washtakiwa watatakiwa ama kuyakana au kukubali mashtaka hayo.
Ikiwa watayakubali, basi mahakama itawatia hatiani na kisha kuwapa adhabu kwa mujibu wa sheria.
Ikiwa watayakana mashtaka hayo, basi upande wa mashtaka utawasomea muhtasari wa maelezo ya kesi. Huu ni muhtasari wa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka, kulinganma na upelelezi.
Kisha washtakiwa baada ya kusomewa maelezo hayo watatakiwa wabainishe mambo wanayokubaliana nayo, yaani mambo yasiyobishaniwa na yale wasiyokubaliana nayo, yaani mambo yanayobishaniwa, ambayo ndio upande wa mashtaka utapaswa kuyatolea ushahidi mahakamani.
Pia, pande zote yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi utapaswa kueleza idadi ya mashahidi pamoja na vielelezo vitakavyotumika katika kesi hiyo, ingawa idadi ya mashahidi inaweza kupungua kadri itakavyoonekana inafaa.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo Februari 16, 2018 katika Viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni na katika Barabara ya Kawawa, Mkwajuni, Kinondoni.
Mbowe kwa upande wake anakabiliwa na mashtaka mengine matano zaidi yeye peke yake, huku Msigwa naye akikabiliwa na shtaka moja zaidi peke yake.
Mbali na mbowe wengine ni Katibu Mkuu, Dkt Vicent Mashinji na manaibu katibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).
Wengine ni mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa; Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake la chama hicho (Bawacha), Esther Matiko na Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee pamoja na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.
Washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 12 ya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali na ya uchochezi wa uasi, wakidaiwa kutenda makosa hayo Februari 16, 2018 wakati wa maandamano yaliyosabasha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.
Wakati kesho vigogo hao wa Chadema watakapopandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuna mambo makubwa mawili yanayotarajiwa kuyojiri katika kesi hiyo.
Jambo la kwanza linalotarajiwa kutokea kabla ya mambo yote ni kuunganishwa nao kwa mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya.
Bulaya ambaye ni mmoja wa washtakiwa katika kesi hiyo, alikuwa bado hajakamatwa na kuhojiwa kabla ya kupandishwa kizimbani kama ilivyokuwa kwa wenzake, lakini April 13, aliitwa Kituo Kikuu cha Polisi na kuhojiwa kabla ya kuachiwa kwa dhamana.
Baadaye Katibu Mkuu wa Chadema, Mashinji alilieleza Mwananchi kuwa mbunge huyo ataunganishwa nao katika kesi yao kesho.
Hivyo, ikiwa kesho atafikishwa mahakamani, basi ataunganishwa na wenzake katika kesi hiyo na katika kufanya hivyo upande wa mashtaka ulazimika kubadili hati ya mashtaka ili kuwasilisha hati ya mashtaka yenye majina ya washtakiwa wote akiwemo Bulaya.
Jambo la pili litakalojiri kesho ni usikilizwaji wa awali wa kesi hiyo. Katika hatua hii upande wa mashtaka utawasomea washtakiwa mashtaka yanayaowakabili na washtakiwa watatakiwa ama kuyakana au kukubali mashtaka hayo.
Ikiwa watayakubali, basi mahakama itawatia hatiani na kisha kuwapa adhabu kwa mujibu wa sheria.
Ikiwa watayakana mashtaka hayo, basi upande wa mashtaka utawasomea muhtasari wa maelezo ya kesi. Huu ni muhtasari wa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka, kulinganma na upelelezi.
Kisha washtakiwa baada ya kusomewa maelezo hayo watatakiwa wabainishe mambo wanayokubaliana nayo, yaani mambo yasiyobishaniwa na yale wasiyokubaliana nayo, yaani mambo yanayobishaniwa, ambayo ndio upande wa mashtaka utapaswa kuyatolea ushahidi mahakamani.
Pia, pande zote yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi utapaswa kueleza idadi ya mashahidi pamoja na vielelezo vitakavyotumika katika kesi hiyo, ingawa idadi ya mashahidi inaweza kupungua kadri itakavyoonekana inafaa.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo Februari 16, 2018 katika Viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni na katika Barabara ya Kawawa, Mkwajuni, Kinondoni.
Mbowe kwa upande wake anakabiliwa na mashtaka mengine matano zaidi yeye peke yake, huku Msigwa naye akikabiliwa na shtaka moja zaidi peke yake.

No comments:
Post a Comment