Katibu wa Bunge atolea ufafanuzi juu ya afya ya Spika wa Bunge. - KULUNZI FIKRA

Wednesday 14 February 2018

Katibu wa Bunge atolea ufafanuzi juu ya afya ya Spika wa Bunge.

 
 Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema hali ya afya ya Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyepo nchini India inaendelea vizuri.

Kagaigai amesema leo Februari 14,2018 kuwa Spika Ndugai yupo India kwa ajili ya kuangalia afya yake (check-up) na anatarajiwa kurejea nchini wakati wowote.

Katibu huyo wa Bunge akizungumza na kulunzifikra blog  iliyotaka kujua maendeleo ya afya ya Ndugai ambaye pia ni mbunge wa Kongwa amesema, “Tulikwisha kusema kwamba Spika yuko India kwa ajili ya ‘check-up’ na hali yake inaendelea vizuri.”

Alipoulizwa kuwa Spika atakuwa ughaibuni hadi lini, Kagaigai amesema: “Hilo ni kati ya daktari wake na yeye lakini ninachoweza kusema wakati wowote anaweza kurudi nchini.”

No comments:

Post a Comment

Popular