Rais John Magufuli wa Tanzania, amefanya mazungumzo na ujumbe wa maseneta wa Baraza la Seneti la Marekani.
Taarifa ya Ikulu ya leo Jumatano imesema maseneta hao ni wajumbe wa kamati ya mazingira inayoshughulikia hifadhi ya taifa, wanyamapori na misitu ya Marekani.
Maseneta hao wamekuwepo nchini Tanzania kwa siku tatu lengo likiwa ni kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.
Mazungumzo hayo pia yamehudhuriwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk Inmi Patterson.
Taarifa ya Ikulu imewataja maseneta hao kuwa ni James Inhofe, Mike Enzi, David Perdue, Luther Strange, Tim Scott na John Thune.
Baada ya mazungumzo, kwa nyakati tofauti maseneta James Inhofe na Mike Enzi wamemshukuru Rais Magufuli kwa kukutana nao.
Pia, wamemshukuru kwa kuwakaribisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Marekani kuja kuwekeza nchini.
Maseneta hao wamesema Tanzania ina rasilimali nyingi ambazo ni fursa muhimu ya kukuza uchumi.
Wednesday, 11 October 2017
Home
Unlabelled
Rais Dkt John Magufuli akutana na Maseneta kutoka Marekani
Rais Dkt John Magufuli akutana na Maseneta kutoka Marekani
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment