Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA, Halima James Mdee, amejibu kauli ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro ya kutojadili suala la Tundu Lissu, na kusema hawatoacha kufanya hivyo.
Kwenye ukurasa wake wa twitter Halima Mdee ameandika ujumbe akisema kwamba hakuna sheria inayokataza mtu kujadili jambo fulani, na IGP hana mamlaka ya kukataza hilo.
“Hakuna popote katika sheria za nchi IGP ana mamlaka ya kunyamazisha watu wasijadili jambo, tutaendelea kujadili ya Lissu mpaka haki itendeke”, ameandika Halima Mdee.
Pia Halima Mdee ameendelea kwa kuandika kuhusu kukamatwa Sheikh Ponda, akisema ni mipango ya kuwafunga mdomo watu watakaojadili suala hilo.
“Najaribu kutafakari alichokisema Ponda na kwa namna gani kinaashiria uchochezi, sikioni! ni namna ya kutisha na kufunga midomo watu”, ameandika Halima Mdee.
Hivi karibuni IGP Sirro aliwataka wanasiasa kuacha kufanya mijadala ya kumjadili Tundu Lissu, na waliache jeshi la polisi lifanye kazi zake bila kuingiliwa na jana Jeshi la polisi lilitoa agizo kwa Shekh Ponda kufika kituo cha polisi kutokana na kauli alizozitoa juu ya sakata la Tundu Lissu.
Saturday, 14 October 2017
Home
Unlabelled
Mdee: IGP Sirro hana mamlaka ya kuzuia mjadala wa tukio la Tundu Lissu
Mdee: IGP Sirro hana mamlaka ya kuzuia mjadala wa tukio la Tundu Lissu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...

No comments:
Post a Comment