Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linamshikilia Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda akituhumiwa kutoa lugha za kichochezi.
Inadaiwa juzi Jumatano, Sheikh Ponda akizungumza na waandishi wa habari alizungumzia masuala mbalimbali ya kisiasa na kutoa taarifa ya kile alichozungumza na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alipokwenda kumtembelea hospitali ya Nairobi nchini Kenya.
Kutokana na kile alichokizungumza, jana Alhamisi, Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alitoa saa 72 kwa Sheikh Ponda kujisalimisha, wito alioutekeleza leo Ijumaa asubuhi akiwa ameambatana na mawakili wanne wakiongozwa na Profesa Abdallah Safari.
Profesa Safari akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoka ndani kwa kupisha swala ya Ijumaa amesema: “Sheikh Ponda wamemshikilia kwa muda, kwani sisi wanasheria wake wote ni Waislamu, tumewaomba twende kuswali tutarejea baadaye,”
“Unajua mimi nimekuwa hapo toka saa 3 asubuhi, tumefanya mahojiano na mdomo, wameweka clip ya kile alichozungumza juzi, wamemwonyesha na ‘Press release’ baadaye wakasema wanaanza mahojiano ya maandishi saa 6.15 mchana sie tukasema twende msikitini kwanza na tukasema tutarudi kama saa 8 au saa 9,” ameongeza:
Kuhusu uwezekano wa dhamana, Profesa Safari amesema hilo litategemea polisi watakavyoamua huku akisema tuhuma zinazomkabili zina dhamana na ni kauli za kawaida ambazo amerejea matukio yaliyotokea.
“Alizungumzia hali ya jumla ya kisiasa, akazungumzia jinsi alivyokwenda kumwona Tundu Lissu…lakini kama wataamua kumshikilia na kutaka kumpeleka mahakamani basi nitaongoza jopo la wanasheria mimi mwenyewe nyani mzee kwenda kumtetea rafiki na mwanaharakati mwenzangu,” amesema Profesa Safari ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara
Friday, 13 October 2017
Home
Unlabelled
Dar es saalm: Jeshi la polisi lamshikilia Sheikh Ponda kwa mahojiano
Dar es saalm: Jeshi la polisi lamshikilia Sheikh Ponda kwa mahojiano
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...

No comments:
Post a Comment