Askofu wa Jimbo Katoliki Zanzibar Agustino Shao, amefananisha Rais Magufuli na Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, kwa uwajibikaji na kukemea vitendo vya rushwa.
Kwenye taarifa iliyotolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari, imeeleza kuwa Askofu Shao ameyasema hayo kwenye ibada ambayo ilihudhuriwa na Rais Magufuli visiwani Zanzibar kwenye kanisa la Mtakatifu Joseph, na kusema kwamba Rais Mugabe alichukua hatua za kupigania maslahi ya Wazimbabwe na sasa hivi wananeemeka na matunda hayo, kitendo ambacho amedai Rais Magufuli anakifanya kwa sasa, na kuwataka watanzania kumuunga mkono.
"Hatutaweza kusema tunaimaliza rushwa wakati tunaendelea kuishi kwa kupata fedha ambazo hatujazifanyia kazi. Ni lazima tuishi machungu ya kuimaliza rushwa. Ni lazima tuishi machungu ya kuweka uadilifu katika utendaji wetu, tusipoishi maisha hayo tutaishi dunia mbili, dunia ya rushwa na dunia ya kujenga uchumi na uadilifu wa watanzania, " amesema Askofu Shao.
katika salamu zake akimshukuru Askofu SHao kwa mahubiri mazuri, amewahakikishia Watanzania kuwa serikali itachukua hatua kupambana na rushwa kulinda rasilimali za nchi, na kuwataka Watanzania wote kuungana katika hilo.
Sunday, 15 October 2017
Home
Unlabelled
Askofu amfananisha Rais Magufuli na Rais Mugabe
Askofu amfananisha Rais Magufuli na Rais Mugabe
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...

No comments:
Post a Comment