Polisi Dodoma limekamata magari 8 na aina ya Nissan Patrol kwa ajili ya uchunguzi wa tukio la kupigwa kwa risasi Tundu Lissu, RPC Muroto asema
Pia jeshi hilo linaendelea kutoa wito kwa wananchi walio taarifa kuwapa ushirikiano ili kuwarahisishia kazi
Amesema tokea tukio la kushambuliwa kwa mbunge huyo dereva wake ajulikanaye kwa jina la Adam bado hajaonekana ila ameona mahojiano yake kwenye gazeti la Mtanzania na kutoa wito kuwa afike ofisi ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Dodoma au ofisi ya mkurugenzi wa makosa ya jinai Dar kwa kuwa wanaamini ana taarifa za siri na kutofika kwake kutawapa mashaka kwamba kuna jambo anaficha
Na sheria kifungu cha 9 na 10 kidogo sehemu ya 2 inasema mtu mwenye taarifa kuhusiana na uhalifu na akakataa kuwapa polisi taarifa hizo atakuwa anatenda kosa la jinai
Pia amesema jeshi la polisi ndilo lenye mamlaka pekee ya kufanya uchunguzi kwenye makosa yote ya jinai na limemekwa na mamlaka na kumtaka Katibu mkuu wa Chadema Vincent Mashinji aliyekuwa akisema anawafahamu waliofanya shambulio hilo kufika ofisi ya mkuu wa upelelezi Dodoma au mkurugenzi wa makosa ya jinai Dar kuwapa maelezo
Pia amesema jeshi lisiingiliwe na tukio hilo lisipelekwe kisiasa na kuchochea wananchi kuichukia serikali yao, matukio mengi yametokea na polisi wamefanikisha kupata wahalifu akitolea mfano matukio ya Kibiti na Mbande na Kongowe ambapo polisi walipoteza maisha
Watuhumiwa wengine 30 wamekamatwa kwa matukio mbalimbali ikiwemo kukutwa na bangi na pombe aina ya gongo
Saturday, 9 September 2017
Home
Unlabelled
Polisi wakamata Magari 8 aina ya Nissan Patrol kuhusiana na tukio la Tundu Lissu.
Polisi wakamata Magari 8 aina ya Nissan Patrol kuhusiana na tukio la Tundu Lissu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

Hayo magari ndio yaliofyatua risasi, hayana wenyewe ?
ReplyDelete