Nyota wawili wa klabu Simba SC, Haruna Niyonzima na Juma Liuzio wameshindwa kufanya mazoezi jioni ya Jana katika uwanja wa Uhuru kutokana na afya zao kutokuwa vizuri.
Wachezaji hao walifika uwanjani hapo kuwashuhudia wenzao wakifanya mazoezi lakini walishindwa kufanya mazoezi kutokana na kusumbuliwa na matatizo tofauti tofauti ya kiafya.
Daktari wa klabu ya Simba SC, Yasini Gembe Amesema kuwa Niyonzima anasumbuliwa na malaria wakati Liuzio akiwa na tatizo la mafindofindo ( tonses) lililompelekea spate homa na kumfanya kushindwa kufanya mazoezi.
Gembe Amesema pia kuwa nyota hao watakuwa wamepata nafuu kabla ya mchezo wa unaofuata wa ligi kuu dhidi ya Mwadui FC utakaofanyika katika uwanja wa Uhuru jumapili ijayo.
"Niyonzima na Liuzio wameshindwa kufanya mazoezi jioni ya Jana kwa vile hawapio fiti ila tunategemea kabla ya mechi ya Mwadui FC watakuwa wamerudi uwanjani" alisema Gembe.
Mshambuliaji Emmanuel Okwi na beki Juuko Murshid ambao walikosekana katika mchezo uliopita dhidi ya Azam FC kutokana na kuchelewa kuripoti kambini wakitokea kwenye majukum ya timu ya Taifa ya Uganda ' The Cranes' walikuwepo kwenye mazoezi.
Tuesday, 12 September 2017
Home
Unlabelled
Niyonzima na Liuzio washidwa kufanya mazoezi
Niyonzima na Liuzio washidwa kufanya mazoezi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment