Hospitali ya Nairobi alikolazwa Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha wanasheria nchini Tundu Lissu imesema haijapokea fedha zozote kutoka bunge la Tanzania hadi kufikia jana saa 10 jioni. Mkuu wa mahusiano ya umma wa KHA inayomiliki hospitali hiyo Bi.Catherine Njoroge ameiambia televisheni ya K24 kwamba hadi kufikia jana malipo hayo yalikuwa hayajafika kwenye akaunti yao.
Catherine alieleza hayo baada ya kuhojiwa na mtangazaji wa K24 aliyetaka kujua kama wamepokea malipo hayo ya TZS 43Milioni sawa na Shilingi 2.1Milioni za Kenya, baada ya bunge la Tanzania kueleza kuwa limefanya malipo hayo tangu jumatano ya tarehe 20 mwezi huu.
"Akaunti iliyotajwa kwenye taarifa ya bunge la Tanzania ni sahihi, lakini bado fedha hizo hazijafika. Kama walituma kwa TT (Telegraphic Transfer) muamala huchukua hadi saa 48 kukamilika. Hivyo kama kweli walituma tunategemea kufikia jumatatu fedha hizo zitakua zimeonekana kwenye akaunti" alisema Catherine.
Saturday, 23 September 2017
Home
Unlabelled
Nairobi hospital: Hatujapokea fedha zozote kutoka Bunge la Tanzania
Nairobi hospital: Hatujapokea fedha zozote kutoka Bunge la Tanzania
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment