Msemaji wa Klabu ya Simba Haji Manara amerusha jiwe gizani na kudai klabu ya Simba ni klabu ya watu ndiyo maana inatajwa kama taasisi maarufu na kudai mtu anayepingana na hilo akapambane na kuwalipa mshahara wachezaji wake.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Manara ameweka ujumbe huo hali ambayo imezua majadiliano huku mashabiki wa Simba na Yanga wakirushiana maneno kutokana na kuwa na upinzani mkubwa kwenye Soka la Tanzania.
"Simba ni klabu ya watu(Peoples Club) watu wa jinsia zote,dini zote, makabila na rangi zote, vyama vyote, ndiyo maana kwa sasa inatajwa kuwa taasisi maarufu kupita zote nchini, ukibisha kapambane na kulipa mishahara wachezaji wako" alisema Manara.
Aidha mashabiki wa soka wengi wamedai kauli ya Manara imekuja baada ya mchezaji wa Yanga ambaye alitokea Simba Ibrahim Ajib kuanza kuonyesha makali yake kwenye mchezo wao wa jana na Njombe Mji kwa kutupia bao 1 huku Simba wakishindwa kuambulia kitu kwenye nyavu za Azam FC katika mchezo wao uliochezwa Jumamosi Septemba 9, 2017.
Monday, 11 September 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment