Wekundu wa Msimbazi Timu ya Simba SC imeshindwa kufurukuta mbele ya timu ya Milambo FC katika mchezo wake wa kirafiki uliopigwa jana katika dimba la Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora ambapo imelazimishwa suluhu.
Katika mechi hiyo iliyochezwa huku mashabiki lukuki wakifurika katika uwanja huo, Simba ilishindwa kuwafurahisha mashabiki wake kwa kuonekana imezidiwa nguvu na timu hiyo ya Milambo inashiriki ligi daraja la pili Tanzania Bara.
Simba ikiwa imewachezesha wachezaji wake nyota John Bocco, Haruna Niyonzima, Mohamed Ibrahim,Laudit Mavugo, James Kotei na wengineo lakini walionekana kuzidiwa ufundi na wakongwe hao wa soka la Bongo ambao wamepotea ligi kuu kwa miongo kadhaa.
Msemaji wa timu ya Simba, Hajji Manara akizungumzia mchezo huo amekubali kiwango kilichooneshwa na Milambo na kubainisha kuwa jicho lao limegundua Milambo kusheheni wachezaji wenye uwezo wa kutosha kucheza ligi kuu .
Monday, 25 September 2017
Home
Unlabelled
Klabu ya Simba SC yabanwa mbavu Tabora
Klabu ya Simba SC yabanwa mbavu Tabora
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetekeleza agizo la Rais John Magufuli kwa kumpatia ulinzi Ana-Joyce Francis, mjane mwenye watoto sita,...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...

No comments:
Post a Comment