JESHI la Polisi mkoani Iringa linamshikilia Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi, Ng’ingula, Wilaya ya Kilolo, Robson Sanga (59), kwa tuhuma za kumua mwanafunzi wa darasa la tano, Emmanuel Gavile (13) kwa kumchapa fimbo mapajani kwa kuchelewa shuleni.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi, alisema tukio hilo lilitokea Agosti 16, mwaka huu saa 3.00 asubuhi shuleni hapo baada ya mwanafunzi huyo kudaiwa kuchelewa kufika shuleni kwa muda ambao shule imeuweka.
Alisema kutokana na adhabu hiyo, Gavile alilia kwa maumivu makali na kushindwa kujisomea hali iliyowafanya wenzake kumkimbiza katika zahanati ya kijiji hicho ambako hali ilizidi kuwa mbaya.
Baadaye alihamishiwa Kituo cha Afya Usokomi wilayani humo.
“Agosti 26 mwaka huu mwanafunzi huyo alihamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa akilalamikia maumivu makali katika paja la mguu wa kulia kabla ya kufariki dunia saa 3.00 asubuhi,” alisema Mjengi.
Kamanda alisema uchunguzi wa daktari umeonyesha kuwa kifo cha mwanafunzi huyo kilisababishwa na kupasuka mfupa wa paja la mguu wa kulia na damu kuviria katika mapafu yake.
Alisema kwa muda wote huo wazazi hawakuweza kuripoti polisi ila baada ya kifo cha mwanafunzi huyo ndipo walipofika kituo cha polisi kutoa taarifa na jeshi hilo limemkamata mwalimu huyo kwa uchunguzi.
Monday 4 September 2017
Home
Unlabelled
Iringa: Jeshi la polisi lamshikilia mwalimu kwa kumchapa mwanafunzi na kusababisha kifo
Iringa: Jeshi la polisi lamshikilia mwalimu kwa kumchapa mwanafunzi na kusababisha kifo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
Wakati leo hii Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiapishwa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete ametoa sababu kushin...
-
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dkt Fredrick Shoo amefunguka na kusema kuwa kama taifa linahitaji maendeleo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Mhe Freeman Mbowe na wenzake wanane ya kutaka kesi dhidi yao ipelekwe Mahakam...
-
Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), Mhe Abdallah Mtolea amefunguka na kuweka wazi kuwa mgogoro uliopo ndani ya Chama chake umekuwa ukiathir...
-
Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto kubwa katika uhitaji wa uzoefu katika nafasi za kazi(work Experience) kwa vijana wa Tanzania. ...
No comments:
Post a Comment