Kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja amefurahishwa na bao alilofunga mshambuliaji wake John Bocco'Adebayor' na kusema kuwa litampa kasi mchezaji huyo ya kufunga zaidi.
Bocco alifunga goli lake la kwanza msimu huu tangu ajiunge na Simba akitokea Azam katika mchezo dhidi ya Mwadui uliofanyika jana na Simba kushinda kwa mabao 3-0. Mabao mengine mawili ya wekundu wa Msimbazi yalifungwa na Emmanuel Okwi.
Mayanja alisema tangu ajiunge na timu hiyo Bocco alikuwa hayuko vizuri kutokana na kusumbuliwa na majeruhi lakini kufunga goli hilo kutamrejesha mchezoni na anaamini atafanya vizuri zaidi katika michezo mingine ijayo.
"Amefunga goli zuri na naamini litampa morali ya kuzidi kufunga katika michezo ijayo. Amekuwa nje ya timu muda mrefu kutokana na majeruhi lakini amecheza mechi mbili na kufunga,ni jambo zuri"alisema Mayanja.
Simba iko nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi saba huku ikiwa timu inayoongoza kwa kufunga mabao mengi kwenye ligi hiyo baada ya kupachika nyavuni mabao 10.
Timu hiyo imeondoka leo alfajiri kwenda Mwanza kupambana na Mbao katika mchezo utakaofanyika Alhamis kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.
Monday, 18 September 2017
Home
Unlabelled
Goli la Bocco Lamfariji kocha Mayanja
Goli la Bocco Lamfariji kocha Mayanja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular
-
THIS ANNOUNCEMENT CONTAINS INSIDE INFORMATION Acacia Mining plc (“Acacia” or the “Company” or the “Group”) Management Changes Ac...
-
Tanzania’s Tunduru district is a major producer of gem-quality sapphire and ruby, along with exotic gems such as alexandrite and tsavor...
-
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii M...
-
Ofisi ya Spika wa Bunge imesema, mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia Chama cha...
-
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge...

No comments:
Post a Comment